Mashahidi wa Lissu - IGP na CDF hawapo nchini, Kingai kuitwa mahakamani Ijumaa
Kesi ya uhaini inayomkabili Tundu Lissu imeahirishwa hadi Ijumaa baada ya mahakama kuelezwa kuwa mashahidi watatu waliotajwa walipelekewa wito lakini walidaiwa kuwa nje ya nchi.